Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ban ataka amani Misri ikipiga kura ya maoni

Ban ataka amani Misri ikipiga kura ya maoni

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon amesema anafuatilia kwa karibu mchakato wa kura ya maoni nchini Misri.

Katika taarifa iliyotolewa na ofisi ya msemaji wa Katibu mkuu mjini New York imemkariri Bwana Ban akisema anasisitiza umuhimu wa kuheshimu uhuru wa kukusanyika na kujieleza pamoja na ahadi ya kutofanya vurugu.

Katibu mkuu amewhamasisha raia wote wa Misri kuhakikisha awamu ijayo ya mpito inafanyika katika njia jumuishi, ya amani na uwazi.

Kadhalika Bwana Ban ametaka raia wan chi hiyo kuelezea tofauti zao bila ghasia huku pia akirejelea uungwaji mkono kwa nchi hiyo kutoka Umoja wa Mataifa katika utawala wa mpito ambao unafuata misingi ya kanuni za kidemokrasia na haki za binadamu kwa wananchi wote wa Msri.