Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ban alaani vikali ongezeko la machafuko Misri

Ban alaani vikali ongezeko la machafuko Misri

Normal

0

false

false

false

MicrosoftInternetExplorer4

st1\:*{behavior:url(#ieooui) }

/* Style Definitions */

table.MsoNormalTable

{mso-style-name:"Table Normal";

mso-tstyle-rowband-size:0;

mso-tstyle-colband-size:0;

mso-style-noshow:yes;

mso-style-parent:"";

mso-padding-alt:0in 5.4pt 0in 5.4pt;

mso-para-margin:0in;

mso-para-margin-bottom:.0001pt;

mso-pagination:widow-orphan;

font-size:10.0pt;

font-family:"Times New Roman";

mso-ansi-language:#0400;

mso-fareast-language:#0400;

mso-bidi-language:#0400;}

Normal

0

false

false

false

MicrosoftInternetExplorer4

/* Style Definitions */

table.MsoNormalTable

{mso-style-name:"Table Normal";

mso-tstyle-rowband-size:0;

mso-tstyle-colband-size:0;

mso-style-noshow:yes;

mso-style-parent:"";

mso-padding-alt:0in 5.4pt 0in 5.4pt;

mso-para-margin:0in;

mso-para-margin-bottom:.0001pt;

mso-pagination:widow-orphan;

font-size:10.0pt;

font-family:"Times New Roman";

mso-ansi-language:#0400;

mso-fareast-language:#0400;

mso-bidi-language:#0400;}

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, amelaani vikali ongezeko la machafuko nchini Misri ambayo yamesababisha vifo vya makumi ya watu na mamia yaw engine kujeruhiwa, kufuatia maandamano mnamo Ijumaa na Jumamosi. Kwa mujibu wa taarifa ilotolewa na msemaji wake, Bwana Ban ametuma risala za rambi rambi kwa familia za wahanga na kuwatakia walojeruhiwa nafuu haraka.

Katibu Mkuu ametoa tena wito kwa mamlaka za mpito nchini humo kuchukuwa kikamilifu wajibu wa kudhibiti maandamano ya amani na kuhakikisha ulinzi wa raia wote wa Misri. Amevitaka vikosi vya usalama vya Misri kuheshimu haki za binadamu kikamilifu katika vitendo vyao, zikiwemo haki za kujieleza na kujumuika, huku akiwasihi waandamanaji kujiepusha na ghasia ili kuendeleza mwenendo wa amani wa maandamano yao.

Taarifa inasema Bwana Ban ametoa wito kwa raia wote wa Misri kushughulikia tofauti zao kwa njia ya mazungumzo, na kutoa wito kwa pande zote kujikita katika harakati jumuishi za maridhiano. Amesema kamwe ghasia haziwezi kuchukua nafasi ya suluhu la kisiasa na hivyo kutoa wito kwa viongozi wote wa Misri kutanguliza matakwa ya taifa lao mbele ya matakwa yao binafsi au vyama na siasa zao.

Bwana Ban amerejelea kusema Bwana Mohammed Morsi na viongozi wengine wa chama cha Muslim Brotherhood ambao sasa wapo kizuizini waachiliwe huru mara moja au kesi zao kuangaliwa kwa njia ya uwazi.