Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hali nchini Mali bado ni tete:UM

Hali nchini Mali bado ni tete:UM

Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanasema hali bado ni tete nchiniMalihuku watu wakiendelea kukimbia na maelfu wakihitaji msaada. Mashirika ya OCHA, WFP na UNHCR, yote yakijitahidi kwa kila njia kuokoa maisha ya mamilioni ya watukamaanavyoarifu Grace Kaneiya.(SAUTI YA KANEIYA)

Mashirika hayo yanatumai kuwafikia mamilioni ya watu kwa msaada wa chakula wakiwemo wakimbizi wa ndani 270,000  na shirika la mpango wa chakula WFP limesema linawafikia watu 310,00 kila mwezi kaskazini mwa nchi hiyo.  

Hata hivyo mashirika hayo yanasema fedha za msaada hazitoshi kukidhi mahitajo yote ya waathirika wa machafukoMali.

OCHA imeanzisha miradi kadhaa  na imetenga dola milioni 16 kutoka mfuko wa dharura CERF kama anavyoeleza Jens Laerke