Syria itoe ushirikiano kwa jopo la uchunguzi wa silaha za kemikali: Ban
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon amezungumza kwenye mkutano wa nchi wanachama wa mkataba wa kimataifa wa kudhibiti silaha za kemikali huko The Hague, na kurejelea wito wake kwa serikali ya Syria kutoa ushirikiano wa kutosha kwa jopo maalum alilounda kuchunguza madai ya matumizi ya silaha za kemikali nchini humo.
Halikadhalika amesema ni matumaini yake kuwa washiriki wa mkutano huo wataibuka na mbinu za kuwezesha matumizi salama ya kemia kwa manufaa ya kiuchumi.