Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

ICC yachukizwa na mwenendo wa vyombo vya habari Kenya kuhusu ushahidi

ICC yachukizwa na mwenendo wa vyombo vya habari Kenya kuhusu ushahidi

Ofisi ya Mwendesha mashtaka mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya uhalifu wa kivita, ICC huko The Hague, Uholanzi imesema inasikitishwa na mwenendo wa kishabiki wa vyombo vya habari nchiniKenyakuhusu hadhi ya mashahidi wa kesi. Taarifa ya ICC imesema ushirikiano wa mashahidi bado ni kipaumbele kikuu cha ICC na kwamba ofisi hiyo haitafuata shuku zozote za umma juu ya hali ya mashahidi. Badala yake imesema ujasiri na uadilifu wa mashahidi ni muhimu mahakama hiyo kupata ukweli ambao ndio kiini cha haki na kwamba ni kwa maslahi ya watu wote kuruhusu sheria kuchukua mkondo wake.