Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ban asifu MONUSCO kupatiwa mamlaka mpya

Ban asifu MONUSCO kupatiwa mamlaka mpya

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon ameunga mkono hatua aliyoitaja kuwa ni muhimu ya Baraza la Usalama kupitisha azimio juu ya Jamhuri ya Demokrasi ya Kongo, DRC ambalo linaipatia ujumbe wa Umoja huo nchini humo MONUSCO mamlaka mpya.

Katika taarifa yake Ban amesema azimio hilo ni hatua madhubuti ya kushughulikia chanzo cha mgogoro Mashariki mwa DRC na Ukanda mzima wa Maziwa Makuu.

Amesema ana imani kuwa azimio hlo litawezesha Umoja wa Mataifa kusaidia utekelezaji wa mpango wa amani, utulivu na ushirikiano uliotiwa saini mwezi Februari mwaka huu huko Addis Ababa na kwamba mjumbe wake maalum kwa nchi za Maziwa Makuu Mary Robinson atashiriana vyema na wadau wote kusongesha mbele mchakato.