Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mashambulizi ya walowezi wa Israeli dhidi ya wapalestina hayakubaliki: UM

Mashambulizi ya walowezi wa Israeli dhidi ya wapalestina hayakubaliki: UM

Mjumbe wa Umoja wa Mataifa katika mpango wa amani wa Mashariki ya Kati, Robert Serry ameeleza kushtushwa kwake na ripoti kuwa walowezi wa kiisraeli wamekuwa wakishambulia mara kwa mara wakulima wa kipalestina katika Ukingo wa Magharibi wa mto Jordan na kuharibu miti ya mizeituni wakati huu wa msimu wa mavuno.

Serry amesema kitendo hicho hakifai na ameitaka serikali ya Israel kuwafikisha mbele ya sheria wahusika wote huku ikizingatia ahadi yake ya kulinda wapalestina pamoja na mali zao. Assumpta Massoi na taarifa zaidi.

(SAUTI YA ASSUMPTA MASSOI)