Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Idadi ya wakimbizi yaendelea kupanda siku za hivi karibuni:UNHCR

Idadi ya wakimbizi yaendelea kupanda siku za hivi karibuni:UNHCR

Zaidi ya wakimbizi 700,000 wameikimbia Syria, Sudan , Mali na Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo tangu mwanzo wa mwaka huu kwa mujibu wa shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR. UNHCR inasema kuwa kuchipuka kwa mizozo mipya na kutotatuliwa kwa ile zamani kumesababisha kuongezeka kwa wakimbizi katika historia yake siku za hivi karubuni.

Kamishina mkuu wa UNHCR Antonio Guterres anasema kuwa uwezo wa mashirika wa kuchukua hatua zinazohitajka unafanyiwa majaribio. Akiongea mjini Geneva bwana Guterees amezishukuru nchi ambazo zimeacha mipaka yao wazi kwa wakimbizi lakini akaomba kutolewa kwa ufadhili zaidi ili kuliwezesha shirika hilo kutimiza majukumu yake.

(SAUTI YA ANTONIO GUTERRES)