Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kuna hatari ya kurejea ukatili wa kimapenzi Mashariki mwa Congo:Wahlstrom

Kuna hatari ya kurejea ukatili wa kimapenzi Mashariki mwa Congo:Wahlstrom

Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu ukatili wa kimapenzi kwenye maeneo ya vita Margot Wahlstrom amezitaka pande zote Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kusitisha mara moja vitendo vyovyote vya ghasia na ameitaka serikali ya nchi hiyo kurejesha udhibiti wake na kuhakikisha raia wanalindwa, katika eneo hilo kutokana na vitendo vya ukatili ukiwemo ubakaji.

Katika taarifa yake Bi Wahlstrom ameelezea hofu yake kuhusu kuendelea kuzorota kwa hali ya usalama Mashariki mwa Congo kufuatia mapigano makali baina ya vikosi vya serikali na makundi ya wanamgambo waasi yenye silaha.

Amesema mashaka yake makubwa ni katika vijiji vya eneo la Walikale Kivu ya Kaskazini ambayo yameghubikwa na makundi ya waasi na yaliyokumbwa na uhalifu mkubwa mwei Julai na Agosti mwaka 2010 ambapo wanawake, wanaume na watoto 387 walibakwa na makundi hayo ya wapiganaji.