UNAIDS na NEPAD watia sahihi makubaliano ya kupambana na ugonjwa wa Ukimwi barani Afrika
Shirika la kupambana na ugonjwa wa ukimwi la Umoja wa Mataifa UNAIDS kwa ushirikiano na shirika la maendeleo la bara Afrika NEPAD wametia sahihi makubaliano ya kutaka kuchukuliwa hatua zaidi katika kupambana na ugonjwa wa ukimwi barani Afrika.
Makubaliano hayo yalitiwa sahihi na mkurugenzi mkuu wa UNAIDS Michael Sidibe na mkurugenzi mkuu wa NEPAD Dr Ibrahim Mayaki mjini Addis Ababa nchini Ethiopia.
Nchi zilizo kusini mwa jangwa la Sahara ndizo zilizo na mzigo mzito zaidi wa tatizo la ugonjwa wa ukimwi duniani.
Mwaka 2010 asilimia 68 ya watu wanaoishi na virusi vya ukimwi walikuwa wakiishi kwenye nchi zilizizo kusini mwa jangwa la sahara eneo lillilo na asilimia 12 ya watu wote duniani.