Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR yasaka dola milioni 157 kusaidia wahanga wa Boko Haram

Mtoto akiwa na hali ya utapiamlo katika kambi ya wamkimbizi wa ndani ya Assaga karibu na mji wa Diffa nchini Niger.

UNHCR yasaka dola milioni 157 kusaidia wahanga wa Boko Haram

Wahamiaji na Wakimbizi

The United Nations High Commissioner for Refugees (UNHCR), along with its humanitarian partners, today launched a $ 157 million fundraising drive to help more than a quarter of a million people affected by Boko Haram attacks in the basin. lake Chad.

Mashirika 47 ya Umoja wa Mataifa na mengine ya misaada ya kibinadamu, ambayo yameungana pamoja katika mkakati wa kikanda kusaidia wakimbizi wa Nigeria wa mwaka 2018-RRRRP yatawajikita kushughulikia mahitaji ya wakimbizi wa Nigeria 208,000 pamoja na wenyeji wao 75,000 katika nchi za Niger, Cameroon na Chad.

 
Akizindua harambee hiyo, katika mji mkuu wa Niger, Niamey, naibu kamishna wa UNHCR, Kelly T. Clements, amesema kuwa mgororo wa Boko Haram umedumu kwa muda mrefu na baado haujamalizika, na hivyo kaiomba dunia kutowasahau waathiriwa  wa mgororo huo mbaya, hususan kukiwa na  matumaini kidogo ya hali kutulia kwa kipindi kifupi kijacho.
 
Wakimbizi kutoka Nigeria wanaendelea kumiminika katika   mataifa jirani. Tangu mgogoro wa Boko Haram uanze  mwaka 2013, watu takriban millioni 2 unusu wamesambaratishwa ndani mwa nchi zao kama vile kaskazini mashariki mwa Nigeria, Cameroon, Chad na Niger.
 
Na moja ya athari za mgogoro huo ni hali inayoongezeka ya uhaba wa chakula na utapia mlo katika maeneo hayo.
Kufikia mwaka 2017 watu katika eneo la bonde la ziwa Chad walikabiliwa na shida kubwa  ya chakula.