Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kuadhimisha Siku ya Maji duniani

Kuadhimisha Siku ya Maji duniani

Katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya maji ambayo kauli mbiu ya mwaka huu ni "maji na usalama wa chakula" inaonekana kuwa nchi nyingi zimepiga hatua katika udhibiti wa maji lakini bado juhudi zaidi zinahitajika.

Mkurugenzi mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO Irina Bokova ameitaka dunia kuungana pamoja ili kuhakikisha kila mtu ana fursa ya maji safi na chakula, sasa na baadaye.

Kwa upande wake Wananchi ambao wengi hukabiliwa na matatizo ya maji wanasemaje kuhusu siku hii.

Hawa ni baadhi ya waakazi wa Afrika Mashariki.

(MAONI KUTOKA AFRIKA MASHARIKI)