UNRWA yazindua ahadi kumi kwa vijana
Mkutano wa kimataifa wa siku mbili wenye kichwa “Kuwashirikisha Vijana: Wakimbizi wa Kipalestina katika kuibadilisha mashariki ya kati” ulioandaliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia wakimbizi wa Kipalestina UNRWA umekamilika hii leo mjini Brussels ambapo kamishina mkuu wa URWA Filipo Grandi amezindua ahadi kumi kwa vijana kwa niaba ya UNRWA.
Mkutano huo ulihudhuriwa na washiriki 400 na washikadau wakiwemo vijana wakimbizi 24 wa kipalestina kutoka Lebanon, Jordan, Syria na eneo la wapalestina lililonyakuliwa.
Kati ya ahadi hizo ni pamoja na kufanya michango ya masomo, mafunzo kwenye nyanja mbali mbali pamoja na fursa za kufikia mashirika ya kifedha.