Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Shirika lisilo la kiserikali lawasaidia waafrika wanaoomba hifadhi marekani

Shirika lisilo la kiserikali lawasaidia waafrika wanaoomba hifadhi marekani

Shirika lisilo la kiserikali lililoko Kaskazini mwa jimbo la New Jersey hapa Marekani liitwalo Begen County Sanctuary kamati kwa ajili ya waoomba hifadhi wa kisiasa linawasaidia waomba hifadhi kutoka Afrika ili kupewa hadhi za kisheria za kuishi nchini Marekani.

Waomba hifadhi hao wanakuja Marekani kutokana na mazingira na sababu tofauti, lakini karibu wote wamekuwa waathirika wa utesaji amesema Dr Joseph Chuman Rais wa shirika hilo. Akizungumza na Radio ya Umoja wa Mataifa amesema wengi wanakuja bila familia zao na kulazimika kuishi katika utamaduni tofauti.

(SAUTI YA DR JOSEPH CHUMAN)