Wafanyakazi wawili wa WFP waliotoweka wapatikana wakiwa salama
Shirika la mpango wa chakula duniani WFP limedhibitisha kuwa wafanyikazi waliokuwa wametangazwa kutoweka wamepatikana wakiwa salama. Wafanyikazi hao walitoweka baada ya kutokea kisa kwenye eneo moja la kisomalia Mei 13 mwaka huu.
WFP imesema kuwa wafanyikazi hao wamesafirishwa hadi mjini Addis Ababa ambapo wanapokea huduma za matibabu na ushauri na kujumuishwa na familia zao. Wafanyikazi hao walipatikana kufuatia ushirikino kati ya WFP na Umoja wa Mataifa pamoja na tawala za kitaifa na kimaeneo.