Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Maelfu ya wahamiaji bado wamekwama nchini Libya:IOM

Maelfu ya wahamiaji bado wamekwama nchini Libya:IOM

Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM linasema kuwa lina mpango wa kuwaokoa maelfu ya wahamiaji waliokwama wakiwemo idadi kubwa ya wanawake na watoto ambao kwa sasa wanahitaji kwa dharura misaada ya chakula na maji , makao na huduma za matibabu baada ya kukaa nje jangwani kwa majuma kadha kusini mwa Libya.

Tayari zaidi ya wahamiaji 2,000 kutoka Chad wamegunduliwa na shirika la IOM kwenye maeneo ya Gatroun and Sebha lakini hata hivyo IOM inasema kuwa huenda idadi hiyo ikaongezeka. Jumbe Omari Jumbe ni afisa wa IOM.

(SAUTI YA JUMBE OMARI JUMBE)