Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wataalamu waliokuwa wanachunguza mafua ya H1N1 watoa ripoti:WHO

Wataalamu waliokuwa wanachunguza mafua ya H1N1 watoa ripoti:WHO

Timu ya wataalamu wa kimataifa ambao wamekuwa wakichunguza hatua za kimataifa za kukabiliana na homa ya mafua ya H1N1 wameandaa ripoti.

Kwa mujibu wa shirika la afya duniani WHO ripoti hiyo inayojumuisha masuala mbalimbali kuhusu hatua zilizochukuliwa na jinsi nchi zilivyokabili mafua ya ndege ya H1N1 hivi sasa imepelekwa kwa nchi wanachama ili kuweza kupata maoni yao.

Timu hiyo ya wataalamu itakutana mjini Geneva na nchi wanachama Machi 28 ili kukamilisha ripoti hiyo baada ya kupata maoni kutoka nchi mbalimbali.