Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Liberia ichukue hatua kuzuia uuzaji haramu wa almasi:UM

Liberia ichukue hatua kuzuia uuzaji haramu wa almasi:UM

Umoja wa Mataifa umesema kuwa Liberia nchi ambayo wakati mmoja ilikumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe imepiga hatua katika kukabilina na biashara haramu ya madini ya risasi, mbao na raslimali zingine ambapo pesa zinatokana na biashara hiyo zimetumika kufadhili vita katika eneo la afrika magharibi.

Kulingana na jopo la wataalamu wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu Liberia ni kuwa taifa hilo linajikokota katika kuchukua hatua zifaazo kulingana na makubaliano ya Kimberley ya kuzua madini ya Almasi yanayotoka kwenye sehemu zinazokumbwa na mizozo.

Madini hayo yamekuwa chanzo kikuuu cha ukosefu wa utulivu barani afrika. Jopo hilo lililobuniwa mwaka 2007 limeitaka Liberia kuwa makini zaidi na kudhibiti uchimbaji na uuzaji wa madini ya Almasi ili kuzuia madini haramu kuingia kwenye madini yaliyo halali.