Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Natija za ubora wa hewa zitasailiwa kwenye Mkutano wa Sayansi ya Angahewa utakaofanyika Korea Kusini

Natija za ubora wa hewa zitasailiwa kwenye Mkutano wa Sayansi ya Angahewa utakaofanyika Korea Kusini

Shirika la UM juu ya Utabiri wa Hali ya Hewa Duniani (WMO) limearifu ya kuwa kikao cha kumi na tano cha Kamisheni juu ya Sayansi ya Angahewa, kitaanzisha mijadala maalumu mnamo siku ya Ijumatano, katika Korea Kusini.