Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

ILO kuwakumbuka waliojeruhiwa na kuuawa kwenye mazingira ya vibarua

ILO kuwakumbuka waliojeruhiwa na kuuawa kwenye mazingira ya vibarua

Shirika la UM juu ya Haki za Wafanyakazi (ILO) limeripoti tarehe 28 Aprili itaadhimishwa kuwa ni Siku ya Usalama na Afya ya Ajira Duniani. Mataifa Wanachama kadha pamoja na mamia ya sehemu mbalimbali za dunia, yatashiriki kwenye taadhima za kuihishimu siku hiyo, zikijumlisha kumbukumbu maalumu za wafanyakazi waliojeruhiwa au kufariki wangali wakiendeleza majukumu ya vibarua walivyoajiriwa.