Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mashirika ya UM yajumuika kukomesha utapiamlo Ethiopia

Mashirika ya UM yajumuika kukomesha utapiamlo Ethiopia

Shirika la WFP pamoja na Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) yamenuia kuisaidia Ethiopia kukabili tatizo la kuviza na kudumaza kwa watoto, tatizo ambalo huchochewa na ukosefu wa lishe bora katika mwili. Mradi huo unatazamiwa kufadhiliwa kutoka msaada wa Kamisheni ya Ulaya (EC) ambayo itajumuika na WFP na UNICEF pamoja na Serekali ya Ethiopia kusaidia wale mama na watoto waliokabiliwa na hali duni kupata huduma za kuboresha lishe na, hatimaye, kuwaepusha vijana na tatizo la kudumaa na kukua na kimo kidogo.