Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Majambazi wavamia malori ya WFP Uganda

Majambazi wavamia malori ya WFP Uganda

Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limeripoti kwamba majambazi fulani walishambulia, kwa kuvizia, msafara wa malori ya UM katika jimbo la Karamoja la Uganda kaskazini-mashariki na kumwua dereva, Richard Achuka, 41, tukio ambalo limeilazimisha WFP kusitisha kwa muda operesheni za kuhudumia waathiriwa wa ukame nusu milioni chakula kwenye eneo husika.