Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wahamiaji 800 kutoka Senegal kuhama makazi na kuelekea Gambia wakikimbia mapigano

Wahamiaji 800 kutoka Senegal kuhama makazi na kuelekea Gambia wakikimbia mapigano

Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limeripoti ya kuwa mnamo wiki mbili zilizopita wahamiaji 800 ziada kutokea jimbo la Casamance la Senegal ya kusini wameyahama makazi yao na kukimbilia vijijini katika taifa jirani la Gambia kujiepusha na mapigano yaliofumka nchini mwao kati ya vikosi vya Serekali na waasi wanaotaka kujitenga, tangu mwezi Agosti mwaka huu.