Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kampeni dhidi ya ujangili ilileta mabadiliko- Kiba

Kampeni dhidi ya ujangili ilileta mabadiliko- Kiba

Mwanamuziki nguli kutoka Tanzania Ali Kiba amesema kampeni ya kulinda wanyamapori ambayo alishiriki akiwa Balozi wa WILDAID ilikuwa ya mafanikio makubwa kwa kuwa ilijenga hamasa miongoni mwa makundi mbali mbali.

Akihojiwa na Idhaa ya Kiswahili kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, Kiba ambaye ameshinda tuzo za kimataifa, kikanda na kitaifa amesema kupitia kampeni mbali mbali za matangazo waligusa hisia za wengi dhidi ya ujangili wa tembo kwa kuwa..

(Sauti ya Kiba)

Amesema kupitia kampeni hizo…

(Sauti ya Kiba)

Lengo namba 15 la malengo endelevu, SDGs linatoa wito kwa jamii na dunia kwa ujumla kushiriki kulinda bayonuai bila kusahau wanyamapori.