Neno la wiki: Aghalabu
Wiki hii tunaangazia neno “Aghalabu” na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.
Aghalab ni kama kielezi na inatumika kumaanisha "mara nyingi, au kwa kawaida au mara kwa mara". Mfano ya matumizi ya neno Aghalab kwa sentensi ni "Nyota nyingi aghalab huonekana usiku" Neno hili lina vinyume vyake kwa mfano nadra, adhimu au mara chache.
Watu wengine hutumia neno hili kimakosa, mara nyingi kumaanisha mara chahe au nadra