Mradi wa UN umenikomboa mimi na familia yangu DRC:Feza Hamis
Mradi wa UN umenikomboa mimi na familia yangu DRC:Feza Hamis
Umoja wa Mataifa umeendelea na kampeni ya kukomesha ukatili na unyanyasai wa kingono katika maeneo yenye mizozo huku ukiimarisha miradi ya kuwasaidia waathirika wa janga hilo. Nchini Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo , DRC Umoja wa Mataifa umewasaidia wanawake wengi waathirika kwa miradi mbalimbali. John Kibego na tarifa zaidi
DRC ambayo bado inaghubikwa na vita kwa miongo kadhaa sasa maelfu ya watu wamefungasha virago kwenda kusaka usalama lakini waliosalia wengine wanakabiliwa na changamoto ya Ebola hivi sasa huku wanawake wengi wakikumbwa na ukatili na unyanyasaji wa kingono na kijinsia. Kwa walionusurika na unyanyasaji wa kingono maisha ni magumu na hata kujikimu wao na familia zao inakuwa mtihani mkubwa.
Lakini sasa kupitia mafunzo ya ujasirimali yanayoendeshwa na mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO na ofisi maalumu ya miradi ya kuwasaidia waathirika wa unyanyasaji na ukatili wa kingono (SEA) kwenye operesheni za ulinzi wa amani, yamewapa matumaini ya maisha wanawake hao na miongoni mwao ni Feza Seluwa Hamisi
SAUTI YA FEZA HAMISI
Na tangu alipopata mafunzo haya hadi sasa Feza anasema mradi huo umekuwa mkombozi kwake na familia yake
SAUTI YA FEZA HAMISI
MONUSCO na ofisi hiyo ya msaada kwa waathirika wa SEA wanasema kipaumbele chao kwa wanawake hawa ni kuhakikisha wanajitegemea na kumudu familia zao .kwa kujiajiri wenyewe kupitia ujuzi wanaoupata ikiwemo wa kuoka mikate, ushonaji, na kilimo.