Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

UN Photo/Manuel Elías

Miaka 75 tumepiga hatua kubwa na tuna ya kujivunia, lakini safari bado ni ndefu:Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema Umoja wa Mataifa una mengi ya kujivunia baada ya kupiga hatua kubwa tangu kuanzishwa kwake miaka 75 iliyopita, lakini bado safari ni ndefu inayohitaji mshikamano wa kimataifa na utashi wa hali ya juu wa kisiasa kukabili changamoto zinazokikikumba kizazi hiki na vijavyo.Jason Nyakundi na maelezo zaidi.

Sauti
3'8"