Mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa lile la kuhudumia watoto UNICEF, na la idadi ya watu UNFP yametangaza leo mjini New York Marekani kuwa, mkakati wa nchi nyingi kutokomeza ndoa za utotoni na kusaidia kulinda haki za mamilioni ya wasichana utafanyika tena kwa kipindi cha miaka minne zaidi.