Wakati mkutano wa kusaka fedha kwa ajili ya Sahel ya Kati unafanyika huko Denmark hii leo, mwanamuziki mashuhuri kutoka Senegal na muungaji mkono wa shughuli za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, Baaba Mal ameandika barua ya wazi kuhusu madhila yanayokumba eneo hilo.