Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

23 Desemba 2021

23 Desemba 2021

Pakua

Hii leo jaridani Assumpta Massoi anaanzia nchini Burundi ambako kijana mmoja baada ya kumaliza masomo ya elimu ya juu na kuona cheti chake hakimpatii ajira aliamua kuanzisha mradi wa kuku na sasa amekuwa chachu kwa jamii yake! Huko Tanzania watoto wamuandikia barua Rais Samia Suluhu Hassan kulikoni? Na kisha ni nchini Mali ambako tofauti za tamaduni zatumika kujenga amani badala ya mvuragano. Makala tunabisha hodi nchini Uganda na mashinani tunakwenda Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kusikiliza faida za rumba!!! Karibu!

Audio Credit
Assumpta Massoi
Audio Duration
14'9"