Wasaidizi wa kibinadamu wa UN Gaza wanahaha, jamii ikikaribia kusambaratika kabisa
Wanawake na watoto wanabeba mzigo mkubwa wa vifo na majeruhi wakati wanajeshi wa Israeli wakipambana na wanamgambo wa Kipalestina katika eneo lote linalokaliwa la Gaza, bila mahali pa usalama pa kwenda, na usambazaji wa misaada ukitatizwa na vita, ukosefu wa kuwafikia wenye uhitaji na uhaba wa vifaa vinavyovuka kuingia katika Ukanda huo yameonya leo mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa.