Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

misaada ya kibinadamu

Familia zinaendelea kupata hifadhi katika makazi ya UNRWA Khan Younis Kusini mwa Gaza
© UNICEF/Abed Zaqout

Wasaidizi wa kibinadamu wa UN Gaza wanahaha, jamii ikikaribia kusambaratika kabisa

Wanawake na watoto wanabeba mzigo mkubwa wa vifo na majeruhi wakati wanajeshi wa Israeli wakipambana na wanamgambo wa Kipalestina katika eneo lote linalokaliwa la Gaza, bila mahali pa usalama pa kwenda, na usambazaji wa misaada ukitatizwa na vita, ukosefu wa kuwafikia wenye uhitaji na uhaba wa vifaa vinavyovuka kuingia katika Ukanda huo yameonya leo mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa.

Watoto wakichota maji huko katika Ukanda wa Gaza
© UNICEF/Eyad El Baba

Hatimaye UNRWA yapokea mafuta

“Kufuatia ucheleweshaji wa wiki kadhaa, Mamlaka za Israel ziimeidhinisha nusu tu ya kiwango cha chini cha mahitaji ya kila siku ya mafuta kwa ajili ya shughuli za kibinadamu huko Gaza.” Amesema Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa Kipalestina UNRWA Philippe Lazzarini

WFP wakiendelea na mpango wa msaada wa chakula nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
WFP/Olivier Nkakudulu

DRC: Helikopta za UN zapakwa rangi ya chungwa ili kuimarisha usalama wa wafanyakazi

Shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya anga UNHAS linalo ratibiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula duniani WFP limeanzisha kundi jipya la helikopta zenye rangi ya chungwa kama sehemu ya juhudi za kuimarisha usalama wa operesheni zake katika eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC ambako mamilioni ya watu wanahitaji misaada ya kuokoa maisha.

© UNICEF/Jean-Claude Wenga

UNICEF: Watoto katika nchi 11 za Mashariki na Kusini mwa Afrika wako hatarini sababu ya kipindupindu

Nchi 11 Mashariki na Kusini mwa Afrika zinakabiliwa na hali mbaya ya mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu ambako hadi sasa kumeripotiwa wagonjwa 67,822 na vifo 1, 788 kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.

Taarifa ya UNICEF iliyotolewa leo mjini Nairobi, Johannesburg na New york inasema huenda idadi kamili ya wagonjwa na vifo ikawa kubwa zaidi kutokana na changamoto ya mifumo ya ufuatiliaji, utoaji taarifa na unyanyapaa.

Sauti
2'21"