03 JUNE 2020
Leo katika Jarida la Umoja wa Mataifa,siku ya baiskeli duniani tutausikia wito wa mwendesha baiskeli.
-Guterres amesema kwamba Corona ni janga la ziada kwa wakimbizi na wahamiaji, tuchukue hatua upya.
- Somalia taifa lililoghubikwa na miongo zaidi ya mitatu ya vita vinavyoendelea sasa mafuriko, nzige na janga la corona vinatishia kurudisha nyuma hatua kubwa zilizopigwa za kisiasa na kiusalama, limeonya shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu masuala ya kibinadamu na misada ya dharura OCHA.
- Na kwenye makala hii leo ikiwa ni siku ya baiskeli duniani, tutausikia wito wa mwendesha baiskeli mmoja jijini Dar es Salaam Tanzania.
- Na leo kwenye mashinani tutakwenda nchini Malawi kuangazia kazi ya Shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia watoto UNICEF pamoja na serikali ya Malawi katika mafunzo ya uongozaji ndege zisizo na rubani.