Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ajira milioni 8 zahitajika ukanda wa Afrika Mashariki kila mwaka- UNECA

Ukanda wa Afrika Mashariki unahitaji kupatia vijana wake stadi sahihi ili kuweza kuziba pengo la ajira.
UN/Eritrea
Ukanda wa Afrika Mashariki unahitaji kupatia vijana wake stadi sahihi ili kuweza kuziba pengo la ajira.

Ajira milioni 8 zahitajika ukanda wa Afrika Mashariki kila mwaka- UNECA

Ukuaji wa Kiuchumi

Ajira milioni 8 zinahitajika kila mwaka katika ukanda wa Afrika Mashariki, ukanda ambao unaelezwa kuwa kasi ya ukuaji wa uchumi ni kubwa mno kuliko kanda nyingine barani Afrika.

Mkutano wa mwaka wa tume ya uchumi ya Umoja wa Mataifa kwa Afrika, UNECA ukiwa umekunja jamvi huko Asmara, mji mkuu wa Eritrea, imeelezwa kuwa kasi ya ukuaji wa uchumi kwenye ukanda wa Afrika Mashariki ni kubwa mno na haiendani na kiwango cha uzalishaji wa ajira, wakati huu ambapo takwimu zinaonesha kuwa ajira milioni 8 zinahitajika kwenye ukanda huo kila  mwaka.

Soundcloud

Kulikoni basi na nini kifanyike? Priscilla Lecomte wa Umoja wa Mataifa ambaye ameshiriki mkutano huo amezungumza na Vincent Leyaro, Mhadhiri wa Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam nchini Tanzania ambaye anaanza kwa kuelezea sababu.