Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

UDSM

© UNICEF/Dhiraj Singh

Ubunifu wetu utasaidia kunusuru bahari- Nancy Iraba

Tukiwa bado kwenye mkutano huo wa Umoja wa Mataifa kuhusu bahari, mbali ya kikao cha ngazi ya juu cha viongozi makundi mbalimbali yalianza kukutana mwishoni mwa wiki likiwemo kongamano la vijana. Nancy Iraba mwanasayansi wa masuala ya bahari kutoka chou kikuu cha Dar es salaam nchini Tanzania ni miongoni mwa wanaohudhuria kongamano hilo la vijana na bahari akiwakilisha taifa lake.

Sauti
1'55"
Picha/Worldreader

Kiswahili chetu ndio hazina yetu

Lugha yako ndio mkombozi wako!  Ikiwa leo ni siku ya Afrika, lugha za asili za Afrika nazo zimepigiwa chepuo na miongoni mwao ni lugha ya Kiswahili ambayo barani Afrika pekee inaongoza kwa kuzungumzwa na watu wengi zaidi, idadi ikitajwa kuwa ni zaidi ya watu milioni 200.

Sauti
2'3"
UNIC Dar es salaam/Stella Vuzo

Wazungumzao Kiswahili ni zaidi ya milioni 200

Lugha za asili barani Afrika zinaangaziwa tarehe 25 mwezi huu wa Mei, ambayo ni siku ya Afrika.

Kuelekea siku hiyo, kumekuwepo na taarifa ya kwamba lugha ya kiswahili ni ya kwanza kwa kuzungumzwa na watu wengi zaidi ikifuatiwa na Hausa halafu Yoruba.

Jambo lililoibua hoja na mjadala mzito kwenye mtandao wa Twitter, si kuongoza kwa lugha hiyo bali ni idadi iliyowekwa ambayo ni milioni 98.

Ili kusaka ukweli wa hoja hiyo nimezungumza na Profesa Aldin Mutembei, kutoka Taasisi ya Taaluma za Kiswahili za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kumuuliza je takwimu ni sahihi?

Sauti
2'3"