Shirika la Umoja wa Mataifa, kwa kushirikiana na serikali ya Somaliland na mradi wa Elimu haiwezi kusubiri, hii leo mjini Hargeisa wamezindua programu ya miaka mitatu ya kuongeza upatikanaji wa elimu bora kwa watoto na vijana walioathiriwa na mgogoro unaoendelea nchini Somaliland.