Kwa miaka mitatu UNA imepata mafanikio makubwa Tanzania:UNA
Umoja wa Mataifa umekuwa na mchango mkubwa katika kushirikisha umma wa Tanzania kwenye harakati za uchagizaji na utimizaji wa malengo ya maendeleo endelevu au SDGs kupitia mbinu mbalimbali ikiwemo mashirika yake na miradi yake. Miongoni mwa mchagizaji mkubwa wa malengo hayo ni UNA.
Jumuiya ya umoja wa Mataifa nchini Tanzania (UNA) imepata mafanikio makubwa tangu kuanzishwa miaka mitatu iliyopita kwa dhamira yakuwa jukwaa la kuchagiza malengo ya maendeleo endelevu SDGs nchini humo na ushiriki wa vijana.
Akizungumza na Stella Vuzo wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa nchini Tanzania , UNIC Dar es salaam wakati wa mkutano wa asasi za kiraria jijini Dar es salaam, Renald Maeda Katibu mkuu wa UNA amesema wameweza kutambua umuhimu wa mchango wa vijana, lakini pia kushirikisha Bunge la nchi hiyo
(MAHOJIANO YA STELLA VUZO NA RENALD MAEDA)