Chuja:

UNIC Dar

24 Julai 2019

Katika Jarida la Habari hii leo arnold Kayanda anakuletea 

-Mikoko yaleta nuru kwa wakazi wa Pwani ya kenya licha ya kuhifadhi mazingira kwa kupunguza hewa ukaa yawaletea kipato wananchi kwa mujibu wa UN Environment

-Vijana nchini Tanzania wakumbatia mabadiliko ya kuachana na matumizi ya mifuko ya plastiki na kujipatia kipato kwa kutengeneza mifuko mbadala ya karatasi

-Elimu katika shule 25 nchini Kenya yapigwa jeki na mradi wa UNICEF wa  vitabu mtandaoni na matumizi ya Ipad

Sauti
13'35"
Photo: IRIN/Mujahid Safodien

Taasisi ya PGWOCADE na harakati za kumkomboa msichana mkoani Rukwa Tanzania.

Mojawapo ya vikwazo vya harakati za kumwinua mwanamke kutoka katika hali duni iliyodumu tangu enzi na enzi mila na desturi za baadhi ya maeneo duniani ambayo wanajamii wamekwenda kwa kasi ndogo katika kuziacha mila hizo kandamizi na potofu. Licha ya ugumu huo, bado mazingira hayo hayapaswi kuwa kikwazo kwa wanarahakati ambao wanahaha kufikia  usawa wa kijinsia kwani mabadiliko ya mila na desturi hayawezi kuwa ya siku moja.

Sauti
4'27"

Malengo ya SDG’s yatamalaki siku ya ushairi duniani

Wakati dunia ikiadhimisha siku ya ushairi duniani hii leo, siku iliyotengwa na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO  kwa lengo la kuchagiza usomaji, uandishi, uchapishaji na ufundishaji wa ushairi, mwaka huu imetoa msukomo katika kuchagiza malengo ya maendeleo endelevu SDG’s.

Tanzania haikusalia nyuma, kwa ushirikiano na kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa nchini humo UNIC wamewashirikisha  washairi kuchagiza SDG’s , shairi la Love Mcharo ni miongoni mwa yaliyotawala, likighaniwa naye Nasir Ibrahim.

Sauti
1'24"