Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tulipokuwa na shida Kenya, Kofi alikuwa nasi hadi suluhu kupatikana- Balozi Macharia

Katibu Mkuu wa UN, Antonio Guterres akiweka sahihi kwenye kitabu cha kumbukumbu katika sherehe ya kumkumbuka  Katibu Mkuu wa zamani  Kofi Annan alieaga dunia 18 Agosti 2018.
UN Photo/Manuel Elías
Katibu Mkuu wa UN, Antonio Guterres akiweka sahihi kwenye kitabu cha kumbukumbu katika sherehe ya kumkumbuka Katibu Mkuu wa zamani Kofi Annan alieaga dunia 18 Agosti 2018.

Tulipokuwa na shida Kenya, Kofi alikuwa nasi hadi suluhu kupatikana- Balozi Macharia

Masuala ya UM

Hii leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa kumefanyika kumbukizi maalum ya Katibu Mkuu wa saba wa chombo hicho, Kofi Annan aliyefariki dunia tarehe 18 mwezi huu wa Agosti huko Uswisi baada  ya kuugua kwa muda mfupi. 

Katika eneo maalum lililopatiwa jina dirisha la amani ambako watu huenda kwa ajili  ya tafakuri na ibada, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anaungana na wafanyakazi wengine pamoja na mwakilishi wa kudumu wa Ghana kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Martha Ama Akyaa Pobee, kuweka saini kitabu cha kumbukumbu na kuweka shada la maua…

Lengo ni kumkumbuka mwendazake Kofi Annan ambaye alianza kazi Umoja wa Mataifa katika ngazi ya chini hadi akakwea na kuchaguliwa kuwa Katibu Mkuu kuanzia 1997 hadi 2006.

Kisha Antonio Guterres akasema..

“Katika zama za sasa za mgawanyiko mkubwa wa kisiasa na mizozo isiyoisha, tunahitaji azma ya kujenga amani kama ya Kofi Annan kuliko wakati wowote ule.”

 

UN /Mark Garten
Balozi Macharia Kamau wa Kenya.(Picha:UM/Mark Garten)

Je kwa waliowahi kufanya naye kazi wanasemaje? Balozi Macharia Kamau, Katibu Mkuu Wizara ya mambo ya nje ya Kenya ambaye amewahi kuwakilisha nchi yake kwenye Umoja wa Mataifa akizungumza na UN News  ameelezea mengi kuhusu mwendazake Kofi Annan na pia kwanini wakenya wanamkumbuka sana.