Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Ghana

Maafisa wa kikosi cha polisi wanawake kutoka Rwanda wakitoa usaidizi kwa kuwatembelea maafisa wenzao waliokwenda kwenye kambi kwa ajili ya kuwasaidia wanawake na watoto wanaoishi kwenye kituo cha ulinzi wa raia Juba , Sudan Kusini
Picha na UNMISS

Wanawake wa Afrika wako msitari wa mbele katika ulinzi wa amani UN

Kuelekea mkutano wa ulinzi wa amani wa Umoja wa Mataifa ngazi ya mawaziri utakaofanyika huko Accra Ghana tarehe 5 hadi 6 Desemba, tunaangazia jukumu la lazima la walinzi wa amani wanawake kutoka Afrika ambao wanakaidi kanuni za kijinsia ndani ya mifumo ya usalama ambayo kwa hulka imekuwa mfumo dume ili kuleta amani na usalama kwa jamii zinazojikwamua kutoka kwenye vita kuelekea katika amani. 

UNICEF Ghana

UNICEF yafanikisha mbinu bunifu za ufundishaji na zimeongeza uelewa wa wanafunzi Ghana

Katika kuhakikisha hakuna mtoto yeyote anayeachwa nyuma kupata elimu Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya watoto UNICEF linatekeleza mradi wa kutoa mafunzo kwa walimu nchini Ghana na tayari wanafunzi 37,000 wamenufaika na mafunzo waliopewa walimu wao. Leah Mushi anatuletea taarifa ya Mwalimu Sam mnufaika wa mafunzo yanayofadhiliwa na UNICEF.

Video ya UNICEF inaanza kwa kumuonesha mwalimu Sam anaendesha baiskeli akielekea shuleni

Walimu Sam anasema yeye ana falsafa yake ya ufundishaji,  

Sauti
1'42"
Watoto darasani wakisoma vitabu vyao katika shule moja  nchini Ghana.
UNICEF Ghana

Mbinu bunifu za ufundishaji zaongeza uelewa wa wanafunzi

Katika kuhakikisha hakuna mtoto yeyote anayeachwa nyuma kupata elimu Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya watoto UNICEF linatekeleza mradi wa kutoa mafunzo kwa walimu nchini Ghana na tayari wanafunzi 37,000 wamenufaika na mafunzo waliopewa walimu wao. Leah Mushi anatuletea taarifa ya Mwalimu Sam mnufaika wa mafunzo yanayofadhiliwa na UNICEF.

Sauti
1'42"
Wakimbizi kutoka Nigeria wakikimbia ghasia huko kaskazini-mashariki mwa Nigeria
© UNHCR/Hélène Caux

Baraza la Usalama shughulikieni mambo haya 5 kusaidia kukabili ugaidi Afrika- Guterres

Hii leo jijini New York, Marekani, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekuwa na mjadala wa ngazi ya juu kuhusu kukabili ugaidi barani Afrika kama hatua muhimu kwa ajili ya amani, usalama na maendeleo ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametaja mambo makuu matano ambayo ametaka Baraza hilo liyazingatie ili kusongesha harakati dhidi ya ugaidi barani Afrika.

Choo kipya nyumbani kwa Agnes Djakwei kwenye mji mkuu wa Ghana, Accra, mradi huu ni wa Benki ya Dunia.
Video ya Benki ya Dunia

Huduma ya choo nyumbani yaleta nuru kwa kaya huko Accra ,Ghana

Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya makazi duniani, ujumbe ukiwa Zingatia pengo lililoko, usimwache  nyuma mtu yeyote au eneo lolote, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anasema ukuaji wa miji lazima uende sambamba na uwekezaji siyo tu wa kuhakikisha kila mtu ana uwezo wa kupata nyumba ya  kuishi bali pia huduma muhimu kama vile za kujisafi, jambo ambalo huko nchini Ghana miradi inayowezeshwa na Benki ya Dunia imesaidia kaya ambazo zamani zilisubiri choo cha umma kisicho kisafi kujisaidia sasa zina huduma hiyo majumbani.

Sauti
2'25"
Clara Magalasi kutoka maeneo ya kijijini ya mji mkuu wa Malawi, Lilongwe alitembea kilometa 4 kuhakikisha mtoto wake Grace mwenye umri wa miezi 22 anapata dozi yake ya nne na ya mwisho ya chanjo ya Malaria.
WHO Malawi

Mpango wa GAVI kuwezesha chanjo ya Malaria kupatikana zaidi Afrika- WHO

Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO kanda ya Afrika, limekaribisha uzinduzi uliofanywa na ubia wa chanjo duniani, GAVI wa fursa kwa nchi kuwasilisha maombi ya fedha ili kuanza kusambaza chanjo dhidi ya Malaria, hatua ambao WHO imesema itawezesha chanjo hiyo kufikia watoto walio hatarini zaidi kwa kuanzia na Ghana, Kenya na Malawi, ambazo tayari zilianza majaribio ya chanjo hiyo mwaka 2019 na hatimaye kusambazwa nchi zingine ambako Malaria imeota mizizi.