Wanawake wa Afrika wako msitari wa mbele katika ulinzi wa amani UN
Kuelekea mkutano wa ulinzi wa amani wa Umoja wa Mataifa ngazi ya mawaziri utakaofanyika huko Accra Ghana tarehe 5 hadi 6 Desemba, tunaangazia jukumu la lazima la walinzi wa amani wanawake kutoka Afrika ambao wanakaidi kanuni za kijinsia ndani ya mifumo ya usalama ambayo kwa hulka imekuwa mfumo dume ili kuleta amani na usalama kwa jamii zinazojikwamua kutoka kwenye vita kuelekea katika amani.