UNHCR kusaidia wakimbizi wa ndani Libya kurejea nyumbani
Baada ya zaidi ya miaka 7 ukimbizini ndani ya nchi yao , hatimaye shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, limeanza kuwawawezesha baadhi ya wakazi wa jimbo la Tawerga nchini Libya kurejea nyumbani.
Bi Amina na mwanae Suhaib ni miongoni mwa zaidi ya wakimbizi wa ndani 40,000 kutoka mji wa Tawergha ambao walilazimika kukimbia vita vya wenyewe kwa wenyewe mwaka 2011 vilivyolipukakatika jimbo la Misrata na vitongiji vyake.
Toka hapo, ni miaka 7 ambapo yeye na jamaa zake wanaishi katika makazi ya kuhamahama ya yaliyopo nje kidogo ya mji mkuu Tripoli.
Sauti ya Amina
Tuliishi katika chumba kimoja kwa zaidi ya miaka 2. Nilipikia humo na kualala humo humo ,mpaka wahisani walipotusaidia.”
Wingi wa watu na ukosefu wa mahitaji muhimu umefanya makazi hayo kukosa hadhi ya kuishi binadamu, hivyo kusababisha UNHCR kuingilia kati ili kuokoa maisha ya maelfu ya wakimbizi wa ndani nchini humo.
Sauti ya Amina
Ni Dhahiri nataka kurudi nyumbani na kuishi Tawergha, ila tuwe salama bila wasiwasi. Sitaki kuona watoto wetu wakitekwa nyara. Na hatutaki kushambuliwa. Ningependa kwenda nyumbani katika hali ya usalama.
Amina anatamani mwanae Suhaib akapaone nyumbani kwao kwa kuwa amezaliwa ukimbizini.
Zaidi ya walibya 180,000 wako ukimbizi katika nchi yao kufuatia migogoro ya kivita inayoendelea nchini humo tangu mwaka 2011 vilivyosababisha Muammar Al Gathafi kuondolewa madarakani.
UNHCR na washirika wake wamekuwa mstari wa mbele kuwawezesha maelfu ya wakimbizi kurejea nyumbani.