Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mchakato wa amani nchini Colombia waanza kuzaa matunda: Arnault

Jean Arnault, mjumbe maalum wa Katibu Mkuu  na mkuu wa ujumbe wa kuhakiki wa Umoja wa Mataifa nchini Colombia,akihutubia baraza la usalama kuhusu Colombia.
UN Photo/Loey Felipe
Jean Arnault, mjumbe maalum wa Katibu Mkuu na mkuu wa ujumbe wa kuhakiki wa Umoja wa Mataifa nchini Colombia,akihutubia baraza la usalama kuhusu Colombia.

Mchakato wa amani nchini Colombia waanza kuzaa matunda: Arnault

Amani na Usalama

Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu na Mkuu wa Umoja wa Mataifa na mkuu wa ujumbe wa Umoja huo nchini Colombia, Jean Arnault amewasilisha ripoti kwenye baraza la usalama la Umoja wa Mataifa hii leo kuhusu mchakato wa amani kati ya serikali ya Colombia na waliokuwa waasi wa kundi la FARC nchini humo.

Katika ripoti yake, Bwana Renauld amesema “licha ya changamoto lukuki , mchakato wa amani nchini Colombia unaendelea kuzaa matunda mazuri na wakati uwakilishi wa FARC katika bunge ni hatua kubwa , ujumuishwaji katika maisha ya kawaida kwa wafuasi wa zamani wa FARC-EP ni shughuli ambayo haijakamilika , akisisitiza kwamba mafanikio ya mchakato huo bila shaka yatahitaji ari na rasilimali.”

Kwa mujibu wa ripoti yake “ lengo kuu la fursa za kuzalishia kipato kwa wapiganaji wa zamani 14,000 bado liko mbali sana kutekelezeka.” Hata hivyo amesema serikali imefanya uamuzi wa kukaribishwa wa kuendeleza msaada wa chakula katika maeneo ya mafunzo na mchakato  wa kujumishwa katika jamii hadi mwisho wa mwaka 2018.

 

Waliokuwa wapiganaji wa FARC wakiwa kwenye mazungumzo na viongozi wa kijami nchini Colombia kama njia ya kujumuishwa tena kwenye jamii.Htua hiyo imewezesha kufanyika kwa uchaguzi mkuu nchini humo
Jennifer Moreno/UN Verification Mission
Waliokuwa wapiganaji wa FARC wakiwa kwenye mazungumzo na viongozi wa kijami nchini Colombia kama njia ya kujumuishwa tena kwenye jamii.Htua hiyo imewezesha kufanyika kwa uchaguzi mkuu nchini humo

Ripoti pia imeainisha masuala mengine ambayo rais mpya mteule Iván Duque atakayeshika hatamu kuanzia Agost 7 mwaka huu atapaswa kuyashughulikia ili kumaliza mgawanyiko miongoni mwa watu wa Colombia. Masuala hayo ni pamoja na makundi mapya haramu, kuendelea kukua kwa biashara ya coca, na ghasia zinazoendelea katika baadhi ya maeneo hususan dhidi ya viongozi wa kijamii na watetezi wa haki za binadamu.