Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UN yashikamana na Pakistan katika vita dhidi ya ugaidi -Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres
UN Photo/Mark Garten)
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres

UN yashikamana na Pakistan katika vita dhidi ya ugaidi -Guterres

Amani na Usalama

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, amelaani shambulio  la kujitoa mhanga lililotokea leo nchini Pakistan.

Shambulio hilo limetokea katika kituo kimoja cha kupigia kura mjini Queatta ambao ni mji mkuu wa mkoa wa Baluchistan.

 Kwa mujibu wa duru za habari takriban watu 31 wameuawa wakiwemo polisi watano na watoto wawili na  wengine 35 wakijeruhiwa.

Shambulio limetokea leo wakati wananchi wa taifa hilo wakiwa kwenye uchaguzi mkuu kuamua nani ataliongoza taifa hilo kama waziri mkuu.

Shambulio hilo limefanyika  baada ya  mtu mmoja kujilipua alipokataliwa na polisi kuingia ndani ya kituo cha kupigia kura.

Katibu Mkuu ametuma salamu za rambirambi kwa familia za waliothirika, watu na  serikali ya Pakistan.

Kupitia tarifa iliyotolewa na msemaji wake, Bwana Guterres amesisitiza kuwa Umoja wa Mataifa unashikamana na kuunga mkono juhudi za serikali ya Pakistan katika vita vyake dhidi ya ugaidi.