Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Huu ni ukatili na unachukiza-UNAMA.

Mji wa Kabul mji mkuu wa Afghanistan
Fardin Waezi/UNAMA
Mji wa Kabul mji mkuu wa Afghanistan

Huu ni ukatili na unachukiza-UNAMA.

Amani na Usalama

Shambulio la kujitolea mhanga katika kituo cha kusajili wapiga kura  katika mji mkuu wa Afghanistan, na kusababisha vivyo vya takriban watu  30 na wengine 50 kujeruhiwa , limelaaniwa na mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Afghanistan, UNAMA.

Shambulio hilo lililotokea leo jumapili mjini Kabul ni la hivi karibuni kati ya mengine mengi yaliyotokea kwa nia ya kulenga  vituo vinavyohusiana na uchaguzi tangu kuanza kwa mchakato wa uchaguzi mkuu wa wabunge na madiwani ambao umepangwa kufanyika  Oktoba 20 mwaka 2018. Mchakato wa kusajili wapiga kura ulianza wiki iliopita.

Mjumbe maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Afghanistan, Tadachi Yamamoto, amesema Umoja wa Mataifa unachukizwa na kukichukulia kitendo hicho kama  cha kikatili. 

Ameongeza kuwa bila kujali maisha ya wananchi,mauaji yaonekana kama sehemu isiyokubalika ya juhudi za wenye misimamo mikali  kuwazuia raia wa Afghanistan kutekeleza haki zao za kikatiba  za kushiriki katika uchaguzi.

Shambulio la leo limefanyika katika kituo cha kusajili wapiga kura kilichoko katika mtaa wa Waislamu wa madhehebu ya Shia ambapo mtu aliejitolea mhanga alijilipua akiwa katika kituo cha kugawa kadi za uchaguzi.

Siku ya Alhamisi, askari polisi wawili waliokuwa katika kituo cha kuwasajili wapiga kura mjini Jalalabad waliuawa kwa kupigwa risasi na watu waliokuwa na bunduki, na wiki iliyopita mjini Ghor, watu waliokuwa na silaha walichoma  kituo cha kuwasajili wapiga kura na kuwachukua mateka maafisa wa uchaguzi na wanausalama. Waliwaachilia siku iliyofuata, na Umoja wa Mataifa unataka waliofanya vitendo hivyo kuchukuliwa hatua za kinidhamu