Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Utoro usipodhibitiwa lengo la elimu itakuwa ndoto Tanzania:

Wanafunzi darasani nchini Tanzania. Picha: UNICEF Video capture

Utoro usipodhibitiwa lengo la elimu itakuwa ndoto Tanzania:

Malengo ya Maendeleo Endelevu

Utoro mashuleni ni moja ya tishio kubwa la kutotimiza lengo namba nne la maendeleo endelevu lihusulo elimu kama hautodhibitiwa nchini Tanzania. Sasa serikali imeamua kulivalia njuga sula hilo kwa kampeni ya mkoa kwa mkoa na mkono wa sheria.

Kampeni hizo ni za kuihamasisha jamii kuelewa umuhimu wa elimu, kuwafikisha mahakamani wazazi wasiohimiza watoto kwenda shule au wanaowafanyika kazi watoto badala ya kuwapeleka shule , lakini pia maandamano ya amani kama yaliyofanyika mkoani Tabora wiki hii na kuhususisha viongozi wa serikali, waalimu, wazazi na wahusika wakuu ambao ni wanafunzi

SAUTI ZA WANAFUNZI

Je hizo ndio sababu pekee za utoro mashuleni? Adda Ezra ni mwalimu  wa shule ya sekondari Ukombozi mkoani Taabora

SAUTI YA MWALIMU ADDA EZRA

Serikali ya Tanzania inasema wazazi wanawajibu mkubwa kuhakikisha watoto wao wanahudhuria shule hivyo imetoa halahala kwa wazazi wasio wajibika kwani mkono wa sheria utawafuata na wameagizwa na mkuu wa mkoa Aggrey Mwanri anayeongoza kampeni hiyo kutii amri la sivyo

SAUTI YA AGGREY MWANRI

Naye mwanasheria mkuu wa mkoa tabora Richard Lugomela akafunguka kuhusu adhabu

SAUTI YA RICHARD LUGOMELA

Kampeni hiyo ya kupinga utoro shuleni na utumikishwaji wa watoto imebeba  kaulimbiu “kamata weka ndani kwa kutotii amri halali” inalenga kuinua kiwango cha elimu mkoani humo, kukomesha utoro  na kuhakikisha lengo la elimu kitaifa linatimia ifikapo 2030. Wanafunzi zaidi ya 11,000 wa shule za msingi na sekondari ni wameorodheshwa kuwa ni watoto sugu mkoani Tabora.