Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Neno la Wiki- Sifongo

Neno la Wiki- Sifongo

Wiki hii tunaangazia neno “Sifongo” na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.

Bwana Sigalla anasema kwamba msamiati huu unafahamika kutokana na kuandikwa sana katika vitabu takatifu. Anasema sifongo ni kama kitu yavu yavu kinachosharabu maji na kina uwezo wa kukaa na maji lakini pia kinayaachia yale maji na hutumika sana kwa kuogea na kujisugulia.