Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mbinu mpya za kilimo zaokoa wakulima Guatemala

Mbinu mpya za kilimo zaokoa wakulima Guatemala

Nchini Guatemala, ukame umekuwa mwiba kwa wakulima, kilimo chao kimekuwa cha mkwamo, wakiwaza kutwa kucha nini cha kufanya ili kunasua maisha  yao. Hata hivyo wataalamu wa kilimo wameibuka na mbinu ya kilimo kinachozingatia mabadiliko ya tabiachi, wakati huu ambapo mkataba wa mabadiliko ya tabianchi ukitaka wakulima nao wasaidiwe ili kilimo kiwe endelevu. Je ni kitu gani wanafanya? Ungana na Assumpta Massoi kwenye makala hii.