Neno la wiki- Falaki
Katika Neno la Wiki hii Septemba 16 tunaangazia neno falaki na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, huko nchini Tanzania.
Neno falaki lina maana zaidi ya moja , ikiwemo elimu ya nyota,pia unajimu maana ya pili ni maisha ya kubahatisha mambo yanayotokea kulingana na elimu ya nyota. Maana ya tatu ni njia ya sayari kama vile jua au mwezi , orbit kwa kingereza na maana ya nne ni anga lote juu tunalolitambua kama mbingu.