Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Afrika yajadili upatikanaji wa maji safi na salama

Afrika yajadili upatikanaji wa maji safi na salama

Mkutano wa sita wa maji kwa bara la Afrika unaendelea jijini  Dar es salaam nchini Tanzania, ukiwaleta pamoja wadau mbalimbali wa maji wakiwamo watafiti na taasisi za miradi ya maji.

Maji na huduma za kujisafi ambalo ni lengo namba sita la maendeleo endelevu SDGs , inatajwa kuwa miongoni mwa changamoto kubwa barani Afrika.

Katika mahojiano na Stella Vuzo wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa  Tanzania, Mtaalamu bingwa wa afya jamii kutoka shirika la afya ulimwenguni WHO Tanzania, Idris Sekibo anaeleza manufaa ya mafunzo na uzoefu unaopatikana katika mkutano huo.

(SAUTI IDRIS)