Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Maofisa polisi Libya wapewa mafunzo juu ya haki za watoto

Nembo ya UNICEF

Maofisa polisi Libya wapewa mafunzo juu ya haki za watoto

Maofisa hamsini wa polisi kutoka nchini Libya wamehitimu mafunzo yao juu ya kukabiliana na vitendo vya unyanyasaji watoto mafunzo yaliyofanyika nchini Tunisia chini ya uratibu wa shirika la UNICEF.

Mafunzo hayo pia yalimulika haja ya maofisa hao kuzingatia sheria za kimataifa zinazolinda haki za mtoto na kuweka mikakati ya kuwaendeleza watoto hao.