UNHCR inasikitishwa na hali ya wakimbizi, serikali yaanza kuwasafirisha kuelekea makambini:Kenya
Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR linasikitishwa na kukamatwa na kuzuiliwa kwa takriban wakimbizi elfu moja na waomba hifadhi waliokamatwa wakati wa operesheni ya kukabiliana na ugaidi inayotekelezwa na vikosi vya usalama nchini Kenya mji mkuu Nairobi tangu mapema mwezi huu ikilenga wakimbizi wasio na vibali.
Wakati hali ya wakimbizi ikiwa sio nzuri serikali ya Kenya imeanza mpango wa kuwafirisha wakimbizi kuelekea kambini. Katika mahojiano maalum na Grace Kaneiya wa Idhaa hii Abel Mbilinyi, Naibu Mwakilishi mkazi wa UNHCR nchini humo anaanza kwa kueleza kile walichoshuhudia katika uwanja wa Kasarani.
(Mahojiano)